SERIKALI imeimarisha
masoko 18 katika jiji la Dar es salaam ili kukabiliana na Ongezeko la Mahitaji
ya Wananchi.
Hayo yamesemwa na Afisa Uhusiano wa Manispaa ya Ilala
Bi Tabu Shaibu wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es
salaam.
Bi Shaibu ameyataja masoko makubwa ni matano
ambayo yameimarishwa kuwa ni
Buguruni,Ilala,Ferry,Kisutu na Mchikichini ambapo jumla ya
wafanyabiashara 8,432 wanatumia masoko hayo.
Akieleza zaidi Bi Shaibu amesema kutokana na
Utafiti uliofanywa na Ofisi ya Biashara ya Manispaa ya Ilala mwaka
2009,ilibainika kuwa jumla ya wafanyabishara 21,500 hawana maeneo ya kufanyia
biashara na wanatumia hifadhi ya barabara na maeneo yasiyoruhusiwa kufanya
biashara.
Kutokana na hali hiyo amebainisha kuwa katika
bajeti ya 2013/2014 jumla ya sh.Milioni 240 zilitengwa kwa ajili ya
ujenzi wa mabanda ya masoko ya Pugu ,Kigogo fresh,Kiwalani na Kinyerezi ambapo
wakandarasi wameshaonyeshwa maeneo ya ujenzi kwa njia ya zabuni.
No comments:
Post a Comment