Tuesday, April 22, 2014

Wabunge , bunge la katika watakiwa kujadili vitu vya msingi ili kupata katiba bora



WABUNGE wa bunge maalum la katiba  wameombwa kuhakikisha  wanajadili vitu vya msingi kwa ajili ya  kufanya kazi waliotumwa na wananchi katika kupata katiba bora kwa maslahi ya watanzania.

Mmoja wa wajumbe hao Bw.  Hamisi Dambaya amesema kuwa katiba mpya haiwezi kupatikana endapo vyama vya siasa vitarushiana vijembe na mwisho kila chama kupita mlango wake na kusema kwamba mpaka sasa mamilioni ya fedha yametumika katika mchakato wa kupata katiba mpya tangu kuanza kwa tume ya Jaji Joseph Warioba hadi kukabidhiwa kwa Raisi.
Naye Mh Catherine Satui amezungumzia suala la muungano na serikali tatu jambo ambalo limeonekana kuzungumzwa kwa kila mjumbe huku mh dokta Harrison Mwakyembe akikemea baadhi ya wajumbe ndani ya bunge hilo maalum la katiba kuwabeza viongozi wenzao.

No comments:

Post a Comment