WANANCHI
wa kijiji cha kiegeya kata ya Berega wilaya ya kilosa Mkoani Morogoro,wameiomba
serikali kuweka jitihada katika kuhakikisha wanaondokana na tatizo la
ukosefu wa maji safi na salama.
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti na Mbiu ya maendeleo,hivi karibuni,wamesema
kuwa tatizo la maji limekuwa la muda mrefu na kwamba waliitikia wito wa
serikali katika kuchangi ili kuweza kupata huduma hiyo jambo ambalo limekuwa
halileti majibu ya uhakika.
Aidha
Wamesema kuwa huamka saa nane za usiku kuwahi maji na hutembea umbali wa
kilomita tano jambo linalowafanya washindwe kufanya shughuli za maendeleo,
ambapo ndoo moja ya maji uuzwa kati ya shilingi 700 na 1000
Nae
Mwenyekiti wa kijiji hicho Bwana John Lucas amekiri kuwepo kwa
tatizo hilo la maji ambapo amesema kuwa kwa sasa wana mpango wa kufadhiliwa na
shirika moja kutoka umoja wa makanisa duniani lijulikalo kama Trufood ambalo
litawajengea bwawa la kuhifadhia maji.
No comments:
Post a Comment