Monday, April 21, 2014

WAKAZIwa manispaa ya Songea watakiwa kubuni mbinu mbalimbali za kukabiliana na ongezeko la taka



MBUNGE wa Jimbo la Songea mjini Mheshimiwa Dokta Emanuel  Nchimbi amewataka wananchi wa Manispaa ya Songea kuwa na tabia  ya kuchukia Uchafu na kubuni mbinu mbalimbali za kukabiliana na ongezeko la Taka kwa kusimamia sheria walizo jiwekea.

Dokta Nchimbi ameyasema hayo jana  wakati akikabidhi magari matatu mawili makubwa kwa ajili ya kuzolea taka na Moja dogo kwa ajili ya matumizi ya Manispaa ya Songea yakiwa yame gharimu kiasi cha shilingi milioni 478.9.

 Amesema msaada wa  Magari hayo umetokana na juhudi za  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete kusimamia maombi ya ufadhili kutoka Benki  ya Dunia akishirikiana na uongozi wa Mkoa wa Ruvuma.

Aidha mbunge huyo  amesema kuwa  pamoja na mradi wa magari kukamilika suala la kuboresha miundombinu ya Maji tayari limepatiwa ufumbuzi kwa kutengewa bilioni moja katika bajeti ijayo, sanjari na  mradi wa ujenzi wa  barabara yenye umbali wa  kilometa 15.




No comments:

Post a Comment