Monday, April 21, 2014

ZOEZI la uandikishaji wa vitambulisho kuendelea jijini Dar es salaam

ZOEZI la uandikishaji wa vitambulisho vya mkazi bado linaendelea jijini Dar es salaam kwa wale wasiojiandikisha, hivyo wananchi ambao bado hawajajiandikisha wamehimizwa kujitokeza kwa wingi ili waweze kupata vitambulisho.
                        
Mkuu wa kitengo cha mawasiliano na hifadhi hati wa mamlaka ya vitambulisho vya Taifa nchini (NIDA)Bwana Thomas William ameyasema hayo hivi karibuni katika mahojiano na mbiu ya maendeleo.

Amesema kuwa wameamua kuendelea na zoezi hilo kwakuwa imebaini  watu wengi hawajajiandikisha na kumekuwa na ongezeko la watu wengi kuhamia katika jiji la Dar es salaam ni vyema zoezi hilo likachukua muda mrefu.
Amesema lengo la vitambulisho ni kutofautisha kati ya watanzania na wasio watanzania.
  



No comments:

Post a Comment