WADAU wa
Maendeleo wakiwemo UNESCO, WHO, UN AIDS, UN,SIDA wameahidi kutoa ya Dola za Marekani 450,000 kwa ajili ya
utekelezaji wa mpango kazi wa maazimio ya wakuu wa nchi 20 , juu ya utoaji wa Elimu ya Afya ya
Uzazi na maadili kwa vijana waliopo katika shule za msingi na sekondari kwa
lengo la kuwawezesha wanafunzi kuepuka mimba za utotoni na kujikinga na
maambukizi ya virusi vya ukimwi.
Akizungumza katika mkutano huo jijini Dar es salaam, Afisa wa
Elimu ya Ukimwi na Afya kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na
Utamaduni UNESCO bwana Mathias Herman amesema katika utekelezaji wa
maazimio hayo, Tanzania inatarajiwa hadi kufikia mwaka 2015 kutekeleza maudhui
ya utoaji wa Elimu ya Afya ya Uzazi kwa wanafunzi wa shule hizo
Amesema Takwimu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
zinaonyesha kuwa , Takriban wanafunzi 6,000 kutoka katika shule za msingi na
sekondari hapa nchini wanaacha masomo kutokana na mimba za utotoni, kutokana na
kukosa elimu ya masuala hayo, ambapo kati ya hao asilimia 40 wanatoka katika
shule za msingi na asilimia 60 wanatoka katika shule za sekondari.
Amesema imebainika kuwa asilimia 50 ya vijana hawana maarifa
ya kutosha juu ya masuala ya afya ya uzazi, hali inayosababisha
vijana hao kuanza mahusiano ya kingono wakiwa na umri chini ya miaka 15
No comments:
Post a Comment