Wednesday, May 28, 2014

UONGOZI wa kiji cha Kivungu wilayani Kilosa ,mkoa wa Morogoro watakiwa kukarabati upya ofisi ya kijiji kutokana na kutokidhi viwango



AFISA  takwimu wa wilaya ya Kilosa Mtila Mbaruku ameuagiza uongozi wa kijiji cha kivungu wilayani Kilosa kukarabati upya ofisi ya kijiji hicho .

Mtila ameyasema hayo ivyi karibuni wakati wa  ziara ya kukagua miradi ya Jimbo la Mikumi na kusema kuwa jengo hilo la ofisi ya kijiji alijakidhi viwango kwani limepauliwa kwa mbao chakavu   lakini pia milango inayotumika aina kiwango .

Aidha ameongeza kuwa Wilaya ya Kilosa ina takribani vijiji 118 ambavyo vinahitaji pesa kwa ajili ya kuanzisha na kurabati miradi mbalimbali lakini kijiji cha kivungu kimebahatika kupata fedha hizo lakini wanavitumia kinyume na malengo .

Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha kivungu Antony Adrian wakati akijibu taarifa ya jengo kuwa chini ya kiwango amekiri mapungufu yaliyopo na kuahidi  kuwa atahakikisha watarekebisha mapungufu yaliyopo katika jengo hilo.

No comments:

Post a Comment