SERIKALI imeshauriwa kuboresha
mifumo ya usajili wa biashara, ili kurahisisha wajasiriamali wengi kusajili
biashara zao na kuliwezesha Taifa kupanua wigo wa ukusanyaji mapato.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Kimataifa ya
Ivestment Climate Facility for Africa (ICF) Bw William Asiko, akizungumza na
wajasiriamali wadogowadogo zaidi ya mia saba waliokutana jijini Dar es
salaam,jana amezishauri mamlaka zinazohusika, kumsaidia mjasiriamali kuondokana
na vikwazo vya kibiashara, sambamba na kuwataka wajasiriamali waliopatiwa
mafunzo kuwa na utamaduni wa kusajili miradi yao ya kibiashara ili waweze
kutambulika kwenye taasisi za kifedha na kuwawezesha kupata mikopo ya
kuendeleza miradi yao..
Kwa mujibu wa taasisi hiyo yenye lengo la
kuondoa vikwazo vya kibiashara kwa wajasiriamali barani Afrika,
inasadikiwa kuna biashara ndogondogo milioni tatu nchini ambazo hazijasajiliwa
kisheria.
Kwa mujibu wa Taarifa rasmi za serikali wakati
wa maadhimisho ya siku ya viwanda Afrika Novemba 20 mwaka jana, sekta ya
wajasiriamali wadogo ina viwanda vidogo vidogo zaidi ya milioni tatu
ambavyo vinaajiri zaidi ya Watanzania milioni 5.2 huku mchango wake katika Pato
la Taifa ukiwa ni asilimia 27 na kwenye ajira ni asilimia 23.4 ya nguvu kazi
yote nchini.
No comments:
Post a Comment