VYAMA
vya
msingi vya ushirika wa wakulima wa kahawa mkoani Kilimanjaro vitaanza
kujiendesha vyenyewe katika shughuli za kukusanya kahawa kutoka kwa wakulima na
kuipeleka sokoni kuanzia msimu huu wa 2014 badala ya chama kikuu cha
msingi cha ushirika cha KNCU.
Meneja mkuu wa KNCU Bw Honest Temba
amesema maamuzi hayo yamepitishwa na mkutano mkuu wa chama hicho ,uliyofanyika
hivi karibuni kwa lengo la kuviwezesha vyama hivyo ,kuendesha shughuli zao kwa
ufanisi zaidi.
Bw. Temba amesema mkutano mkuu umependekeza kuwa
,ili wakulima na vyama hivyo viweze kunufaika na kilimo cha kahawa ,KNCU
itavijengea uwezo vyama hivyo kwa kuvipatia elimu ya kujiendesha ,hususani
katika biashara ya kahawa pamoja na kusimamia fedha zao wenyewe sambamba
kukabiliana na changamoto mbalimbali.
No comments:
Post a Comment