Wednesday, May 7, 2014

JAMII imeombwa kutoa ushirikiano kwa wakunga ili kuhakikisha mama wajazito wanapata huduma stahiki



JAMII na serikali imetakiwa kutoa ushirikiano kwa wakunga kwa lengo la kuhakikisha kuwa mama wajawazito wanapata huduma stahiki toka kwa wataalamu hao wa afya ili kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Nasaha hizo zimetolewa hivi karibuni na Raisi wa chama cha wakunga nchini Dk Fredy mwanga katika maadhimisho ya siku ya wakunga duniani yaliyofanyika mnazi mmoja  jijini Dar es salaam.

Dk Mwanga Amesema kuwa, kuna baadhi ya wakunga wanakiuka maadili ya kazi kwa kutoa lugha chafu kwa kina mama wajawazito wanapotoa huduma hali inayopelekea wananchi kuwachukia baadhi yao na kuilahumu serikali ilihali ukunga ni taaluma inayoongozwa kwa maadili ya kazi kama zilivyotaaluma nyingine.

Kutokana na hali jamii imeombwa kutoa taarifa kwa waganga wakuu wa hospitali za wilaya na mkoa sanjari na vituo vya afya endepo patatokea udhalilishaji toka kwa wakunga ili sheria ichukue mkondo wake..

No comments:

Post a Comment