KUSHAMILI kwa ujangili katika hifadhi za Taifa zilizopo
hapa nchini kunasababisha kupungua kwa watalii kuingia kwa wingi
kutokana na baadhi ya wanyama pori kutoweka na kuziacha hifadhi hizo
kutokuwa na wanyama wa kuvutia.
Akizungumza katika mdahalo ulioandaliwa na Umoja wa wanafunzi
wanaosomea mambo ya wanyamapori katika Chuo Kikuu cha Kilimo Cha
Sokoine,Afisa masoko kutoka Bodi ya Utalii nchini Bwana Peter Mkumbo
amesema sababu kubwa ya kupungua kwa watalii hapa nchini inatokana
na kuongezeka kwa ujangili katika hifadhi hizo.
Aidha Bwana Mkumbo amefafanua kuwa kupungua kwa hoteli za kulala
watalii pia ni sababu moja wapo ya kupungua kwa watalii nchini ambapo kwa sasa
wanamikakati ya kuhamasisha wawekazaji kuwekeza katika maeneo hayo ili
kulisaidia Taifa kuongeza watalii na kuongeza kipato.
No comments:
Post a Comment