Thursday, May 29, 2014

HALMASHAURI ya wilaya ya Kilosa yashauriwa kutenga fedha zaa kutosha kwaajili ya fedha za maendeleo



HALMASHAURI ya Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro imeshauriwa kutenga fedha za kutosha katika Bajeti ya mwaka wa fedha 2014/2015 kwa ajili ya miradi ya maendeleo na kumtuma mkaguzi kukagua matumizi ya fedha za mfuko wa jimbo zilizotumika kwenye miradi wilayani humo.
Ushauri huo umetolewa mapema leo na kamati za mifuko ya jimbo zilipokuwa zikifanya majumuisho ya ziara ya kukagua miradi inayokarabatiwa kwa fedha za mifuko ya jimbo la Kilosa na Mikumi Wilayani humo.

Akitoa taarifa kwa  vyombo vya Habari katibu wa mifuko ya jimbo Mtila Mbaruku amesema zaidi ya miradi 22 imekaguliwa ambapo jimbo la Kilosa kati miradi 14 na Mikumi ni miradi 8 na kwamba baadhi ya miradi imejengwa chini ya kiwango kutokana na kamati za vijiji kuwa na matumizi mabaya ya fedha.
Akizungumzia miradi iliyojengwa chini ya kiwango , ameitaja kuwa ni pamoja na vyumba viwili vya madarasa katika shule ya msingi kitunduweta  na mradi wa barabara ya Mabura Mafera yenye  urefu  wa kilomita tano ambayo imekarabatiwa chini ya kiwango hali  iliyopelekea  kusombwa  na maji na kusababisha wananchi kushindwa  kusafiri kwa haraka wanapopatiwa matatizo.

Kutokana na hali hiyo Mtila amewataka viongozi wa serikali za vijiji kusimamia kikamilifu matumizi ya fedha zote za serikali zinazopelekwa kwenye vijiji vyao kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

No comments:

Post a Comment