Thursday, May 29, 2014

KATIBU wa chama cha UDP mkoa wa Morogoro afariki Dunia




KATIBU wa chama cha United Democratic Party UDP mkoa wa Morogoro Ununi Mn’goo(61) amefariki dunia jana nyumbani kwake kijiji cha Kikundi baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa UDP Mkoa Dominick Ponela,Katibu huyo alikuwa akisumbuliwa na Maralia ya vipindi sambamba na vidonda ndani ya kifuani.........

.Ponela alisema tayari amewasiliana na makao jmakuu ya chama hicho jijini Dara es salaam na ofisi imeahidi kushiriki mazishi hayo yanayotaraji kufanyika kijijini hapo leo majira ya jioni.

Mng'oo ambae ni miongoni mwa waasisi wa chama hicho Mkoani Morogoro na nchini pia aliwahi kuwa mwalimu wa shule ya msingi,Mratibu elimu kata ya Tegetelo,Katibu wa utamaduni wilaya na mwenyekiti wa asasi binafsi ya Tushikamane.

Kwa mujibu wa ndugu wa karibu wa marehemu marehemu alikuwa na wake wawili akiwemo aliyefunga nae ndoa ya dini,mwingine aliyefunga ndoa Bomani sambamba na watoto nane.


No comments:

Post a Comment