BAADA ya Halmashauri ya wilaya ya Kilosa kutoa idhi kwa wanakijiji cha Mbigili kitongoji cha Mateteni kugawana ardhi ya Mwekezaji Mees Estate Ltd kwa madai kuwa imefutiwa umiliki wake,uongozi uliowekeza katika ardhi hiyo umeibuka ukilaani vikali kitendo hicho na kudai fidia ya shingi Mil.800.
Mbele ya waandishi wa habari mjini
Morogoro mmoja wa wakurugenzi wa Mees Estate Ltd inayomiliki mashamba ploti
namba 28,29 na 32, Patrick Mees alisema chokochoko hizo dhidi ya mashamba hayo
yenye ukubwa wa ekari 1,466 zimesababisha kushusha uzalishaji mwaka huu na
kuamsha hofu dhidi ya uhai wao na mali shambani hapo.
“mashamba haya tunayamiki kihalali
kwa hati ya umiliki ya 1987 na tangu kipindi hicho tunayatumia kuzalisha zaidi
ya tani 25,000 za aina mbalimbali za nafaka ukiwemo Mpunga na Mahindi licha ya
uwekezaji mwingine kama Majengo,mifugo,majosho na msitu wa miti ya Mbao aina ya
Mkongo” alisema
Juzi wakiongozwa na mwenyekiti wa kamati ya
Ardhi wilayani humo Anna Sanga,Afisa ardhi wilaya Arnold Selestine na
Mwanasheria wilaya Ocate Maganiko walifika ktongoji cha mateteni na kuuagiza
uongozi wa kijiji hicho kugawana mashamba ploti namba 28,29 na 32.
Kwa mujibu wa viongozi hao kijijini
hapo,uamuzi wa halmashauri hiyo kugawa shamba hilo unatokana mashamba hayo
kufutiwa umiliki wake na rais mwaka 2000 kisha kurejeshwa kwa wananchi.
No comments:
Post a Comment