MPANGO wa kuwasaidia
mikopo wanaume waliofiwa na wake zao (WAGANE) umeanza kufanyika
katika kata za MBUMI na KASIKI katika mamlaka ya mji mdogo wa Kilosa,mkoani Morogoro.
Akizungumza mapema leo na Mbiu
ya maendeleo kwenye kata ya Mbumi Afisa maendeleo ya jamii wa kata hiyo
Bi Avintishi Abdallah amesema kuwa mchakato huo umeanza ambapo
kwenye kata hiyo wameshapokea wagane 8.
Bi Abdala ameeleza kuwa ili wagane
hao waweze kunufaika na mkopo huo wanapaswa waunde vikundi kwa watu wasiopungua (5) huku akiwahimiza wagane waliopo katika kata hiyo kujitokeza kwa wingi ili waweze kufaidika na mikopo hiyo
itakayosaidia kujiletea maendeleo na kuendelea kulea vyema familia zao.
No comments:
Post a Comment