JUMLA ya mbwa 70 wamepatiwa chanjo katika tarafa ya Kilosa mjini,wilayani Kilosa, mkoa
wa Morogor oili kuwakinga na ugonjwa wa kichaa cha mbwa
Akizungumza na mbiu ya maendeleo mapema leo mjini Kilosa, Afisa
wa mifugo wilaya
Dokta David Shemweta amesema zoezi hilo limeusisha kata nne za
tarafa ya Kilosa mjini ambapo kutokana na idadi hiyo ndogo ya mbwa waliopelekwa
na wamiliki wao kupatiwa chanjo hiyo zoezi ilo litafanyika tena wiki ijao
ya mei 31 mwaka huu ili kuwapa nafasi ambao mbwa wao hawajapatiwa chanjo .
Ameongeza zoezi hilo la chanjo cha kichaa cha mbwa hufanyika
kila mwaka mara moja ikiwa ni pamoja na kutoa dawa ya minyoo ambayo hutolewa kila baada ya
miezi mitatu ambapo amesema kuwa iwapo mbwa asipopatiwa chanjo ya kichaa cha
mbwa mara ang’atapo mtu hupata ugonjwa wa kichaa cha mbwa .
No comments:
Post a Comment