Saturday, May 24, 2014

WIZARA ya elimu na mafunzo ya ufundi yapewa changamoto



CHANGAMOTO imetolewa kwa wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi  kuhakikisha kuwa wananchi wanapatiwa elimu ya kutosha  kuhusu kuongezwa kwa alama za ufaulu kupitia vipindi vya elimu kwea umma kwa njia ya redio na runinga.

Wakiongea na Mbiu ya maendeleo jijini Dar es salaam jana katika banda la Baraza la mitihani la Taifa( NECTA)  kweny e kilele cha maonesho ya vyuo vikuu, badhi ya wananchi wamesema kuwa, kushambuliwa sana kwa wizara ya elimu kuhusu alama za ufaulu ni kutokana na kitengo cha elimu kwa umma kutokuwa na vipindi , hivyo wakati umefika kwa wizara husika kuondoa sintofahamu hiyo ndani ya jamii.

Wamesema jamii hasa wadau wa elimu wamekuwa na mtazamo hasi kuhusu kuongezwa alama na madaraja ya ufaulu kutokana na kukosa ufafanuzi toka mamlaka husika.

Asilimia kubwa ya wananchi waliotembelea maonesho hayo walikuwa wananchi wa liomaliza kidato cha nne na sita ili kupata ushauri na ufafanuzi kuhusu mambo mbalimbali yanyohusu vyuo vya ndani na nje ya nchi.


No comments:

Post a Comment