MBUNGE wa Jimbo la
Kilosa Mustapha Haidi Mkulo ameamua kutoa dukuduku lake la muda mrefu kabla
ajafa kuwa hakuusika wala hakushiriki katika mchakato wa kuuza kiwanja
no. 10 cha shirika Hodhi la mali za serikali (CHC) wakati alipokuwa waziri wa
fedha nchini.
Mkulo amesema hayo hivi karibuni
wakati akizungumza na wazee wa jimbo
lake juu ya tuhuma iliyomkabiri ya uuzwaji wa kiwanja hicho kilichotajwa
kuwa kiliuzwa kinyume cha utaratibu kwenye ripoti ya mwaka 2010/2011 na
mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) .
Mkulo amesema kuwa tangu apate
tuhuma hiyo hakuwai kupata nafasi yoyote kwenye ngazi za serikali ili aweze
kutetea juu ya tuhuma hiyo na kwamba ameamua kuliweka wazi kwa wazee wake wa
baraza katika jimbo la Kilosa kuwa hakuhusika kwenye mchakato mzima wa uuzwaji
wa kiwanja hicho.
Amesema kuwa si yeye tu hakuhusika
hata wizara yake ya fedha pia haikuwa ikihusika na kuongeza kuwa wakati kiwanja
hicho kinauzwa yeye alikuwa nchini Marekani kwa majukumu mengine ya
kitaifa.
Sambamba na hayoMbunge huyo amesisitiza
kutangaza kuwa anastahafu siasa na hatakuwa tayari kugombea tena ubunge ifikapo
2015 ni katika kutimiza azma ya kuwa mbunge kwa vipindi viwili bali sasa
ataendelea kuwa mwanachama wa kawaida.
No comments:
Post a Comment