BUNGE limeendelea kujadili makadirio ya bajeti ya
wizara ya uchukuzi mjini Dodoma kwa baadhi ya wabunge kuchangia mjadala
wa wizara hiyo.
Awali
akiwasilisha maoni ya kambi ya upinzani Mheshimiwa Moses Machali ameishutumu
serikali kwa ufisadi wa matumizi mabaya ya fedha zinazotolewa na
serikali kwa miradi mbalimbali.
Aidha
amesema kuna matumizi mabaya ya madaraka serikalini,yanayo sababisha
dhuluma na ufisadi, akitolea mfano manyanyaso ya faini wanazotozwa
waendesha pikipiki nchini maarufu kama bodaboda yanayofanywa na mamlaka
husika.
Kwa upande
wake mbunge wa bariadi mashariki mheshimiwa Andrew Chenge ameishauri serikali
kupitia wizara ya Uchukuzi isiitegemee benki ya Dunia katika kutekeleza
majukumu yake hasa katika utekelezaji wa miradi mbalimbali pia ameiomba
serikali iachane na visingizio vya muda mrefu kwa wizara hiyo juu ya upembuzi
yakinifu na usanifu kwa miradi hiyo.
Ushauri
mwingine umetolewa na mheshimiwa James Mbatia ambapo yeye kwa upande wake
amesema Serikali ifanye maamuzi magumu katika kutekeleza majukumu yake kuliko
kubaki na hali ya kushuka na kupanda katika miradi yake.
No comments:
Post a Comment