Monday, May 26, 2014

SHIRIKA la Compassion Tanzania latoa msaada wa vyandarua



JUMLA ya vyandarua 260 vyenye thamani ya shilingi milioni mbili na themanini elfu vimetolewa na shirika la compassion Tanzania kituo cha 552 kwa kushirikiana na kanisa la Moravian usharika wa Morogoro mjini.
Akizunguza katika hafla hiyo  ya kutoa vyandarua hivyo kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi na yatima,mchungaji wa kanisa hilo bwana Lawi Mwankuga ameitaka jamii kuvitumia vyandarua hivyo kwa malengo yaliyokusudiwa na kuacha kuvitumia  kwa ajili ya kufugia kuku na mambo mengine ambayo yanarudisha nyuma juhudi za kupambana na ugonjwa wa malaria

Kwa upande wake Mkurugenzi wa compassion Tanzania  wa kituo cha 552 bi Josephine Donald amesema wafadhili wa shirika hilo wameamua kujinyima kwa kidogo walichonacho ili kuwasaidia watoto wa kitanzania waishi katika mazingira yaliyobora huku bwana Bonifani Nyangala akisema kuwa msaada huo umetolewa wakati muafaka ambapo taifa limekumbwa na ugonjwa wa Dengue.

Shirika la compassion Tanzania lilianzishwa mwaka 2004 ambapo kwa sasa limetimiza miaka kumi na tatu tangu kuanzishwa kwake limekua likitoa huduma  mbalimbali kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi ikiwemo  elimu,afya pamoja na huduma za kiroho


No comments:

Post a Comment