Monday, May 26, 2014

UJENZI wa shule ya sekondari ya Iwemba ,wilayani Kilosa wafikia asilimia 85



JUMLA  ya shilingi milioni mbili laki tano na elfu sabini na tano zimetumika katika ujenzi wa vyumba vitano vya nyumba ya mwalimu katika shule ya sekondari ya Iwemba iliyopo katika kata ya kidodi wilayani Kilosa mkoani Morogoro .

Hayo yameelezwa na afisa mtendaji wa kijiji cha Iwemba bwana Jonasi Adamu Mathias wakati akitoa taarifa ya ukarabati wa mradi huo kwa wajumbe wa mfuko wa jimbo la kilosa hivi karibuni .

Bwana Mathias  amesema kuwa kati ya fedha hizo zilizotoka katika mfuko wa jimbo la Kilosa ni shilingi milioni mbili laki sita na elfu themanini na nane na nyingine shilingi laki tatu na elfu tisini zimetolewa na wananchi ambapo fedha hizo zimetumika katika upauwaji ,kuweka dali ,umeme ,lipu pamoja flow katika nyumba hiyo .

Amesema kuwa mradi huo wa nyumba umeanza kutekelezwa tangu mwezi wa nne mwaka huu ambapo  unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi wa sita kwasasa ujenzi huo   umekamilika kwa asilimia 85 .




No comments:

Post a Comment