JUKUMU la kuleta
maendeleo katika jamii halina budi mwenda sanjari na wananchi kutoa ushirikiano
kwa wataalamu,Imeelezwa.
Mtaalamu wa lishe toka Chuo kikuu
cha kilimo cha Sokoine cha mjini Morogoro Bwana Mnyika Stewart ameeleza hayo
mapema jana katika mahojiano maalum na Mbiu ya maendeleo jijini Dar es salaam
katika ukumbi wa Diamond Jubilee.
Amesema wananchi wengi hawatoi ushirikiano wa kutosha
kwa wataalamu hasa katika masuala ya
ufikishwaji wa taaluma na teknolojia mbalimbali za afya hali inayopunguza ari na moyo kwa baadhi ya wataalamu.
Kutokana na hali hiyo ametoa wito kwa
maafisa maendeleo ya jamiii na uongozi wa kata na wilayani kutoa elimu ya mara
kwa mara ili kuleta mabadiliko chanya ndani ya jamii.
No comments:
Post a Comment