Saturday, May 24, 2014

WANANCHI wilayani Kilosa wametakiwa kusimamia kikamilifu miradi ya maendeleo



KATIBU wa mfuko wa jimbo la kilosa kati Mtila Mbaruku amewataka viongozi wa vijiji vilivyoko kata ya kidete wilayani Kilosa kusimamia kikamilifu mradi wa ukarabati wa visima vya maji kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wa vijiji hivyo.

Akizungumza may 23 mwaka huu Mtila Mbaruku ambaye pia ni Afisa wilaya ya Kilosa katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika kata ya kidete na Lumuma iliyojumuisha ukarabati wa visima vine vya maji amesema kuwa wananchi wanapaswa kufahamu kuwa visima hivyo vya wananchi wa vijiji hivyo.

Amesema kuwa visima hivyo vinakarabatiwa kwa kutumia fedha za mfuko wa jimbo baada ya mbunge wa jimbo la Kilosa kati Mustapha Haidi Mkulo kuona umuhimu kuwapelekea maji wananchi wa vijiji hivyo kutokana na shida ya maji wanayoipata.

Amesema kuwa Mkulo amenunua vifaa vya kukarabati visima vya vijiji vya kitati , mwasa, manolowe  na mzaganza ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi kwa wananchi wa kata ya Kidete wakati wa kampeni  za uchaguzi wa mwaka 2010.

Hata hivyo Mtila amewataka wananchi kuhudhuria kwenye mikutano ya kijiji ili kuwasilisha na kuibua hoja za miradi ya maendeleo na kupata majibu sahihi kutoka kwa viongozi wao  na siyo kutoa lawama zisizo kuwa na msingi kwa viongozi wa ngazi za juu.


No comments:

Post a Comment