Saturday, May 24, 2014

SERIKALI imetakiwa kuweka maeneo maalum ya malisho ili kuepusha sintofahamu kati ya wakulima na wafugaji



KUKOSEKANA kwa maeneo yaliyopimwa kwaajili ya wafugaji imeelezwa ndio sababu inayochangia migogoro sugu ya wakulima na wafugaji nchini.

Hayo yameelezwa leo bungeni mjini Dodoma na mbunge wa Meatu kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo chadema Mheshimiwa Meshack Opulutwa wakati akichangia bajeti ya wizara ya mifugo  na Uvuvi.

Amesema , mifugo inachangia pato kubwa la nchi na baadhi ya mikoa inayotegemea mifugo ambapo alitoalea mfano wa mkoa wa Simiyu amabo umepata shilingi  bilioni 27 mwaka 2013/2014 kutokana na mifugo ikiwa na watu milioni 1.5 na ng’ombe milioni 2 huku ikipata maziwa lita milioni 21 kwa mwaka



No comments:

Post a Comment