SERIKALI inakabiliwa na ukosefu wa maafisa
ugani mia sita kukamilisha idadi kamili
inayotakiwa ili kuwafikia wananchi katika maeneo mbalimbali nchini.
Waziri wa
mifugo na Uvuvi Dokta Titas Kimani ameelza hayo bungeni mjini Dodoma wakati
akiwasilisha bajeti ya wizara yake.
Amesema idadi
kamili ya maafisa ugani wa sekta ya uvuvi wanaotakiwa nchi nzima ni 1500 wakati waliopo kwa sasa ni mia tisa.
Hata hivyo
waziri huyo wa mifugo amesema , jitihada mbalimbali zinafanyika katika
kukabiliana na hali hiyo ikiwemo kuongeza udahili wa wanafunzi wa kozi za uvuvi
katika vyuo mbalimbali vya uvuvi nchini kwa ngazi za astashahada, stashahada na
shahada ya kwanza.
No comments:
Post a Comment