Friday, May 23, 2014

SERIKALI yaahidi kuwezesha elimu ya juu nchini.



 SERIKALI imeahidi kuwa itaendelea kutekeleza majukumu yake katika kuwezesha elimu ya juu nchini kuwa yenye ubora na viwango vya kimataifa kaaajili maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Hayo  yamebainishwa mapema leo na waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi   Mheshimiwa Sshukuru Jumanne Kawambwa wakati akifunga maonesho ya tisa ya vyuo vikuu yaliyoandaliwa na tume ya vyuo vikuu nchini (TCU)katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.

Waziri Kawambwa amesema kuwa, serikali imefungua milango kwa watu na Taasisi binafsi kufungua vyuo vikuu  ili kuharakisha maendeleo  ili nchini na jukumu la serikali litakuwa kuwapatia msaada wa mikopo kwa wananfunzi wanaojiunga na vyuo vikuu hivyo.

Katika maonesho hayo ya vyuo vikuu nchi kumi na moja zimeshiriki mwaka huu ambapo vyuo vikuu ishirini toka nchini China vimeshiriki.

No comments:

Post a Comment