Friday, May 23, 2014

SHIRIKA la kiraia wilayani Kilosa latoa msaada wa kisheria kwa wananchi



SHIRIKA  la kiraia la Morogoro paralegal limetoa Mafunzo ya usaidizi wa kisheria kwa wananchi wapatao 25 wa Wilaya Kilosa,mkoani Morogoro  ambao watasaidia jamii masikini katika kupata haki zao katika vyombo vya kutolea maamuzi.

Akiongea na waandishi wa habari wilayani mjini Kilosa mapema leo,Mkurugenzi wa shirika hilo la Morogoro paralegal centre for women and children , Frola Masoy amesema kuwa lengo la kutoa mafunzo hayo ni kutoa msaada wa kisheria kwa jamii isiyo na uwezo kifedha na haiwezi kumudu gharama ya kumtumia wakili wa kumsaidia kupata haki.

Masoy amesema pindi wasaidizi wa sheria watakapokamilika kupata mafunzo hayo wananchi wa hali ya chini wataweza kupata haki zao tofauti na sasa wanadhurumiwa kwa kukosa msaada wa kisheria na pia itasaidia kupunguza kesi Mahakamani.

Kwa upande wao, wananchi wanaopatiwa mafunzo hayo wamelishukuru shirika hilo kwa kuwapatia mafunzo hayo kwani ni mambo yanayotokea katika jamii hivyo wamehaidi kuisaidia jamii kupata haki zao.










No comments:

Post a Comment