KAMATI ya Ardhi ya
kugawa mashamba Wilayani Kilosa,mkoani Morogoro imekabidhi mashamba kwa serikali ya kijiji cha
Mbigili kilichopo kata ya Magole wilayani humu zaidi ya hekari 1466 kwa ajili
ya kuwagawia wananchi wa kijij hicho kwa ajili yashughuli za kilimo.
Akizungumza na mwandishi wetu
mapema leo Afisa Ardhi na mali asili wilaya Bwana Ibrahimu Ndembo amesema
kuwa mashamba hayo ambayo yamekabidhiwa kwa serikali ya kijiji yalifutwa na
Rais Jakaya Kikwete umiliki kutoka katika kampuni ya MES ESTATE LIMITED mwaka 2000.
Ndembo amesema kuwa baada ya Rais
Kikwete kufuta umiliki wa mashamba hayo no. 28 ,29 na32 kutoka kwa mmiliki wa
kampuni hiyo kutoka Dar es salam kikao cha kugawa Ardhi cha wilaya
kiliamua mashamba hayo yagawiwe kwa wananchi ili kuondoa mgogoro wa muda mrefu
kati ya wananchi na mmiliki wa kampuni hiyo ambaye alileta sintofahamu kati yake na wanakijiji ikiwa ni
pamoja na kuwapeleka mahakamani baadhi yao kwakila mwananchi aliyekuwa akifanya
za kilimo katika shamba hilo.
Amesema kuwa baada ya kamati hiyo
kuwakabidhi hekari hizo za mashamba serikali ya kijiji hicho cha Mbigili
imewataka kuhakikisha mpaka kufikia
tarehe moja mwezi wa sita mwaka huu wahakikishe wameshawagawia wananchi
maeneo ya kilimo na ikipendekeza kuwa kitongoji cha Mateteni kipewe
kipaumbele kwani akina eneo kwa ajili ya kilimo .
No comments:
Post a Comment