MKUU wa wilaya ya
Kilosa,mkoani Morogoro Elias Tarimo
amemtaka mwenyekiti wa chama cha wakulima wa miwa MSINDAZI CANE GROWERS
ASSOCIATION (MCGA) kilichopo Ruaha wilayani humo,Bwana Ayubu Mora kuendelea na madaraka mpaka
muda wake utakapo kwisha ili atatuwe changamoto zinazokikabili chama hicho.
Tarimo ametoa kauli hiyo hivi
karibuni kwenye mkutano mkuu wa wakulima na viongozi wa chama hicho uliohusu
kusomewa taarifa ya ukaguzi na mapato na matumizi ya chama mwaka 2009 hadi 2014
.
Tarimo amemtaka kiongozi huyo
kuendelea na madaraka kutokana na mgogoro ulioko kati ya wanachama na viongozi
wa chama hicho juu ya deni la jumla ya zaidi ya shilingi milioni mia moja
arobaini zinazodaiwa baada ya kukopa kutoka kwa wanachama , wahisani, na Bank
ya CRDB kwa ajili ya kununua gari la kupakia miwa (Cane loader).
Awali mwenyekiti Ayubu Mora
aliwataarifu wanachama kuwa baada ya kusomewa taarifa ya mapato na matumizi
atajiudhuru na kujiondoa katika nafasi hiyo ili uchaguzi wa muda ufanyike
,ndipo wakulima waliibua hoja mbalimbali juu ya uhai wa chama na kusema kuwa
endapo mwenyekiti huyo atajiudhuru viongozi wengine na wanachama
wataondoka katika chama hicho hivyo kupoteza uhai wa chama .
No comments:
Post a Comment