Tuesday, May 27, 2014

WAZIRI Tibaijuka atembelea wilaya ya Mvomero kukagua mipaka katika vijiji vilivyomo wilaya humo



WAZIRI wa ardhi , nyumba na maendeleo ya makazi jana ametembele wilaya ya Mvomero,Mkoani Morogoro kwa lengo la kukagua mipaka katika vijiji vilivyopo wilayani humo.

Katika ziara hiyo Waziri Tibaijuka amezungumza na wananchi wa kijiji cha Lukenge na kusema kuwa suala la kusimamia ardhi linahitaji umakini ili kuepuka migogoro inayotokana na ardhi.

Prof Tibaijuka amesema  kuwa vijiji 31 vimeandaliwa  kwa ajili ya kupimwa na vingine nane  vinahakikiwa huku akiwaagiza wakulima na wafugaji kundelea kuishi kwa amani kwani mfugaji ana haki ya kufuga na mkulima anayo haki ya kulima.

Awali akisoma Risala kwa niaba ya wanakijiji wa Lukenge Afisa Mtendaji wa kijiji hicho bwana Ally Kingu amesema wanaishukuru serikali kwa kukarabati jengo la Masjala ambalo limegharimu kiasi cha shilingi milioni sita laki nane na ishirini elfu ambapo waziri Tibaijuka amelifungua rasmi wakati wa ziara yake.

Kijiji cha Lukenge kina jumla ya Ng’ombe elfu nne na mbuzi zaidi ya elfu tatu ambapo katika ziara hiyo pia waziri Tibaijuka alitembelea shamba la mfano la ukulima wa nyasi kwa ajili ya malisho.
                              

No comments:

Post a Comment