Tuesday, May 27, 2014

MKUTANO wa siku mbili wa bodi ya usajili wa makandarasi nchini kuanza kesho



BODI ya usajili wa makandarasi inayosimamia shughuli zote za ukandarasi nchini, inatarajiwa kufanya mkutano wa siku mbili kujadili ufanisi wa Makandarasi katika majukumu yao pamoja na kuangalia mamlaka zinazosimamia shughuli za makandarasi.

Akizungumza na waandishi wa habari,jijini Dar es salaam,mwenyekiti wa bodi ya makandarasi,bwana Boniface Muhegi, amesema mkutano huo pia utatathmini changamoto zinazowakabili makandarasi na namna ya kuzitatua pamoja na kuboresha utendaji wao, ukiambatana na maonesho ya makandarasi na vifaa vya ujenzi.

Sambamba na hilo amesema katika mkutano huo, wahandisi ambao hufanyakazi na makandarasi wataapishwa kudumisha maadili ikiwemo kutoshiriki vitendo vya rushwa pamoja na kusimamia kazi zao kwa weledi ili kuwaimarisha  kazi zao.

No comments:

Post a Comment