Akiongea na Mbiu ya Maendeleo mjini Morogoro mapema jana ,mganga mkuu wa hospitali hiyo Daktari Hores Msacky amesema tulimpokea mtoto huyo akiwa katika hali ya uchafu usio wa kawaida na tuliamua kumfanyia vipimo vya awali pamoja na picha za X ray, ambaapo imegundulika kuwa mifupa yake inaonekana imevunjika ingawa hawajajua nini kimemvunja.
. Hata hivyo Msaky alisema kuwa hospitali hiyo haina vifaa vingi vya kupimia mifupa, hivyo mtoto huyo atapelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu zaidi.
Muuguzi katika Wodi ya watoto hospitali ya rufaa ya Morogoro akimuhudumia
mtoto Nasra Said mara baada ya kufikishwa hopsitalini hapo kupatiwa
matibabu.
Baba mzazi wa mtoto huyo alisema yeye ana mke na watato wengine wa ndoa na
kwamba hakuwahi kumwambia mkewe kama ana mtoto wa nje hivyo ilikuwa vigumu
kumchukua mtoto huyo na ndipo alipomkabidhi mama mkubwa wa mtoto huyo.
Mtoto Nasra akiwa katika wodi ya watoto hospitali ya mkoa wa Morogoro
anakopatiwa matibabu kwa sasa.
Baada ya kufikishwa katika kituo cha polisi mwanamke huyo alikiri kuanza
kumlea mtoto huyo tangu akiwa na umri wa miezi tisa na kwamba hatua hiyo
ilikuja baada ya mama yake, kufariki dunia mwaka 2010.
Hata hivyo majirani hao walidai wanahusisha tukio hilo na imani za
kishirikina kutokana na kwamba mama huyo anaakili timamu na analea watoto wake
vema tofauti na mtoto huyo.
No comments:
Post a Comment