KAMPUNI
ya uchimbaji Madini ya African Barrick inayomiliki Mgodi wa North Mara imelipa
kiasi cha Dola laki nane sawa na shilingi Bilioni 1 na milioni mia 300 kwa
halmashauri ya wilaya ya Tarime Mkoani Mara ikiwa ni tozo ya huduma kwa kipindi
cha Mwaka 2002 hadi 2005.
Makabidhiano
hayo yamefanyika katika baraza la Madiwani la halmashauri ya wilaya ya Tarime
mkoani Mara mbele ya Naibu waziri wa nishati na Madini mheshimiwa Steven
Masele.
Bw Masele
amesema kuwa pamoja na kukamilika kwa Malipo hayo mgodi huo unatakiwa
kukamilisha yale yote ambayo wamekubaliana ikiwa ni njia ya kuondoa malumbano
ya mara kwa mara kati ya Mgodi na viongozi wa halmashauri hiyo.
.
Kwa Mujibu
wa Naibu waziri Masele mpaka sasa halmashauri nne hapa nchini
zimelipwa Tozo ya huduma ambayo ni Shilingi Bilioni 8 kutoka katika Makampuni
ya Migodi iliyopo katika halmashauri hizo huku viongozi wa halmashauri ya
Tarime wakiahidi kuelekeza fedha hizo katika Miradi ya Maendeleo.
No comments:
Post a Comment