RAISI wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete amemteua Bwana Rished BADE kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA).
Kulingana na Katibu Mkuu
Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, uteulzi huo umaanza tangu Mei sita
mwaka huu ambapo Bwana BADE anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bwana Harry
KITILYA ambaye alistaafu Desemba 14,mwaka jana.
Kabla ya uteuzi huo,
Bwana BADE alikuwa Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania tangu
Septemba,2012 na baadaye kukaimu nafasi ya Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato
Tanzania tangia Bwana Kitilya alipostaafu.
Kabla ya kujiunga na
Mamlaka ya Mapato Tanzania, Bwana Rished BADE amewahi kufanya kazi katika maeneo
mbalimbali yaliyompa ujuzi na weledi mkubwa kwenye mambo ya fedha na mapato.
Mheshimiwa Rais
ana imani kubwa kwa elimu, uzoefu na weledi alionao, Bwana Rished Bade kwa
kushirikiana na watumishi wenzake, katika kutoa mchango kwa Taifa na
kuzidi kuimarisha Mamlaka hiyo na kuboresha utendaji wake na hivyo kuongeza
mapato ya Serikali kwa faida ya Taifa.
No comments:
Post a Comment