MKUU wa wilaya ya Mvomero mkoani
Morogoro bwana Antony Mtaka amesitisha shughuli za uzalishaji na
ujenzi wa wa kiwanda cha madini katika kijiji cha Melela Mlandizi baada
ya mwekezaji kubainika kutofuata taratibu za kisheria.
Bwana
Mtaka ametoa kauli hiyo wakati wa mkutano wa viongozi na wanakijiji ambao
wameulalamikia uongozi wa kijiji hicho kufanya mikataba pasipo kuwashirikisha
wananchi.
Amesema
uongozi wa wilaya umebaini kuwa mwekezaji amepewa ardhi kinyume cha taratibu
ambapo maombi yaliishia kwenye halmashauri ya kijiji pasipo kuthibitishwa
na idara za madini,ardhi,mazingira na ridhaa ya wanakijiji.
.
Hata
hivyo amemtaka mwekezaji huyo kufika ofisi ya mkurugenzi mtenda wa halmashauri
ya wilaya ya Mvomero ili kupata barua yenye nukuu za kisheria kutoka wizara ya
madini ili imsaidie kupata uhalali wa kupata leseni, ridhaa ya wanakijiji na
kumwezesha kufanya shughuli zake kihalali.
No comments:
Post a Comment