WAKULIMA nchini wametakiwa kuwa karibu na wataalamu wa
Kilimo ambao watawasaidia katika masuala mbalimbali ya kilimo yatakayoweza
kuwanufaisha ili kuepukana na kilimo kisichokuwa na tija.
Ushauri
huo umetolewa jana na Meneja Masoko wa
kampuni ya uzalishaji mbegu za nafaka SEEDCO,bwana Sillas Ngowe wakati wa
maadhimisho ya siku ya wakulima iliyofanyika katika kijiji cha Vikenge
kilichopo Kata ya Mzumbe wilayani Mvomero mkoani Morogoro.
Siku
ya wakulima katika kijiji cha Vikenge wilayani Mvomero mkoani Morogoro
imeandaliwa na kampuni ya uzalishaji mbegu za nafaka ya Seed Co kwa
kushirikiana na kampuni za Bayer,Opportunity,Syngenta pamoja na wakala wa
usambazaji pembejeo za Kilimo mkoani Morogoro Imuka Agricultural Enterprises.
No comments:
Post a Comment