Wednesday, May 21, 2014

ZAIDI ya tani 24,000 za sukari zimedoda katika kiwanda cha Illovo wilayani Kilombero


SHEHENA yenye zaidi ya tani 24,000 za Sukari imedoda katika maghara ya Kiwanda cha Sukari ILLOVO Kilombero na kuhatarisha ajira za wafanyakazi kiwandani hapo samnbamba na kukua kwa umasikini wilayani Kilombero.

Kudoda kwa shehena hiyo kunkwenda sambamba na lawama dhiidi ya serikali kudawiwa kuruhusu kwa holele kuingizwa kwa Sukari nyingi kutoka nje ya nchi inyouzwa kwa bei nafuu tofauti na inayozalishwa nchini.

Mbele ya Naibu waziri wa Kilimo,chakula na Ushirika Godfrey Zambi, Kaimu mkurugenzi mkuu wa kiwanda cha Ilovo Joseph Rugaimukamu na Mwakilishi wa Bodi ya Sukari nchini Abdul Mwankemwa walisema mbali na hujuma hiyo wafanyabiashara wanatumia mifuko yenye nembo ya viwanda vya nchini kujaza sukari ya nje.

Walisema hujuma hiyo imesababisha viwanda kushindwa kulindwa kwa kuruhusu shehena za bidhaa hiyo kuingizwa nchini hivyo makampuni ikiwemo Illovo kushindwa kujiendesha na kuelemewa na mzigo wa madeni ya wafanyakazi,wakulima na taasisi nyingine zikiwemo za kifedha.

"iwapo TRA hawatadhibiti hali hii kuna hatari viwanda vingi vikajifunga kwa kushindwa kujiendesha baada ya bidhaa zake kukosa soko"alifafanua Rugaimukamu. 



No comments:

Post a Comment