Wednesday, May 21, 2014

SHIRIKA la world vision latoa mafunzo ya ujasiriamali wilayani Kilosa


SHIRIKA  la world vision lililoanzishwa mwaka 1959 nchini Marekani na kuingia nchini Tanzania mwaka 1980 leny elengo la kuleta ustawi wa mtoto kuwa na maisha mazuri, Afya njema na kumjua mungu , limetoa mafunzo ya ujasiriamali kwa vikundi vya vikoba wilayani kilosa.

Katika mafunzo hayo yaliyohudhuriwa na wajumbe kutoka katika vikundi mbalimbali katika kutoa mafunzo hayo wamewezeshwa jinsi ya kuendesha vikundi vyao na taratibu na kanuni za kufuata katika kuendesha vikundi vyao.

Naye meneja wa mradi wa Ulaya ADP katika shirikala  world vision Mathias Mwingila amesema kuwa katika kutoa mafunzo hayo wanakumbana nachangamoto mbalimbali ikiwemo baadhi ya wanavikundi kudai posho wakati wanapoitwa kupewa mafunzo na kusema kuwa lengo la world vision n ikutoa mafunzo ya kuweza kujikwamua kimaisha na kuleta maendeleo katika jamii.

Aidha ameongeza kuwa changamoto nyingine ni mapokeo hasi kwa baadhi ya wajumbe wakidhani kuwa world vision inaeneza dini ya kikristo kutokana na shirika hilo kuanzishwa na watu wa dini ya kikristo na amebainisha kuwa shirika hilo halipo upande wowote wakidini ila lipo kwaajili ya kutoa mafunzo ya kujikwamua kimaisha kwa wajasiriamali wadogowadogo.







No comments:

Post a Comment