Saturday, May 3, 2014

SHIRIKA la kuhifadhi misitu ya asili lahamasisha jamii kujiunga na vikundi



SHIRIKA la kuhifadhi misitu ya asili Tanzania (TFCG)  kupitia mradi wa  kuongeza thamani katika misitu AVA limeanza kuhamasisha jamii zinazoishi kando kando ya misitu kujiunga katika vikundi vya hisa ili kupunguza  uharibifu wa mazingira.

Hayo yameelezwa na Meneja wa Mradi wa AVA Bwana Hassan Chikira na kusisitiza kuwa mradi huo unatekelezwa  katika vijiji 31 vilivyomo katika wilaya ya MVOMERO mkoani Morogoro.

Bwana Chikira amesema uanzishwaji wa vikundi hivyo kupitia mradi wa AVA utawarahisishia wananchi wanaoishi kando ya misitu kupata fedha za kuendesha miradi mingine na kuacha kutegemea misitu kama chanzo cha mapato yao.
 .
Mradi wa AVA umelenga kuhakikisha jamii inayozunguka misitu inaacha tabia ya kutumia misitu kama chanzo cha kipato ili waweze kuhifadhi   mazingira.



No comments:

Post a Comment