UMOJA wa wanawake wa
Chama Cha Mapinduzi (UWT) mkoani Mara, Umekemea vikali na kulaani matukio
ya mauaji dhidi ya wanawake yanayoendelea katika maeneo mbalimbali katika mkoa
huo.
Tamko la kulaani mauaji hayo limesomwa jana na katibu mkuu wa UWT
mkoa wa Mara Bi. Hellena Chacha katika ukumbi wa CCM mkoani Mara kwa niaba ya
mwenyekiti wa umoja huo Bi. Nancy Msafiri.
Amesema mauaji hayo ya kikatili yasiyo na kikomo kwa wilaya ya
Butiama yanalaaniwa kwa nguvu na UWT mkoani Mara na kuiomba serikali kuchukua
hatua katika kukomesha mauaji hayo na kuifanya Butiama kuwa kanda Maalum ya
kipolisi.
.
Mauaji ya wanawake katika mkoa wa Mara yamekuwa yakitokea
mara kwa mara na hivyo kutishia uwepo wa tatizo la njaa kutokana na wanawake
hao kushindwa kwenda shambani ambako ndiko wauaji hutekeleza azma zao hizo
ikihusishwa na vitendo vya kishirikina.
No comments:
Post a Comment