Saturday, May 3, 2014

ZAIDI ya watu 1500 wanaoishi kinyume cha sheria wamekamatwa nchini Kenya



MKAKATI maalum wa kuwasaka magaidi na majambazi nchini Kenya umekamata zaidi ya watu 1500 wanaoishi kinyume cha sheria nchini humo.

Mkuu wa jeshi la polisi nchini Kenya IGP David Kimaiyo ameeleza hayo mapema jana wakati akiongea na vyombo vya habari kuutaarifu ulimwengu hali halisi ya msako huo ambao ni endelevu  mpaka hapo hali itakapokuwa shwari.

Kamanda Kimaiyo  amesema watu hao 1500  waaliokamatwa katika opresheni wanatoka nchi mbalimbali za Afrika ikiwemo Tanzania, Somali, Uganda, Burundi na Sudani.
Ameafafanua kuwa waliorejeshwa ni wale ambao hawana vibali vya kisheria vya kuishi nchini Kenya na hakuna ubaguzi katika operesheni hiyo.

No comments:

Post a Comment