VIONGOZI
wametakiwa kuwajibika na kuwa waadilifu ili kuhakikisha kuwa
wanawaletea maendeleo wananchi kkatika muda muafaka.
Mbunge wa jimbo la Ubungo Mheshimiwa John Mnyika
ametoa rai hiyo mapema jana katika kikao cha kujadili ujenzi wa Zahanati ya mtaa wa Malamba mawili kata ya Msigani jimbo
la Ubungo,jijini Dar es salaam.
Mheshimiwa Mnyika amefafanua kuwa ni jambo la busara
kwa wananchi kushirikiana na viongozi kiujiletea maendeleo huku wakisubiri
serikali kutekeleza ahadi iliyo waahidi wananchi wake.
Katika kikao hicho Mheshimiwa Mnyika alichangia
shilingi milioni kumi kwaaajili ya ujenzi wa Zahanati ya Mtaa wa Malamba mawili
kata ya Msigani ,Manispaa ya Kinondoni , jijini Dar es salaam.
No comments:
Post a Comment