Sunday, May 4, 2014

SHULE za msingi nchini zinakabiliwa na upungufu wa madawati yapatayo milioni moja na nusu



WAZIRI MKUU Mheshimiwa Mizengo Pinda amesema shule za msingi hapa nchini zinakabiliwa na upungufu wa madawati yapatayo milioni moja na nusu ambapo ameitaka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ijifunge mkanda na kulipa kipaumbele suala la kupunguza tatizo hilo.

Waziri Pinda metoa agizo hilo jana wakati akiwahutubia mamia ya wakazi wa Mkoa wa Dodoma ambao walihudhuria uzinduzi wa Wiki ya Elimu Tanzania kwenye uwanja wa Jamhuri.

 Kutokana na mahitaji hayo, Waziri Mkuu amesema endapo Serikali itaamua kutengeneza madawati 100,000 kwa mwaka kwa gharama ya sh. bilioni 12/ itachukua miaka 15 kumaliza tatizo hilo ili kuziba pengo lililopo sasa.

Mheshimiwa Pinda amesema ni lazima hatua madhubuti zichukuliwe kumaliza tatizo hilo kwani inatia aibu na hakuna sababu ya kuendelea kuona wanafunzi wakisoma huku wamekaa chini.
 Wakati huohuo, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Profesa Idris Kikula, akitoa shukrani kwa niaba ya wadau wa elimu alisema anaunga mkono hoja ya uchangiaji wa madawati na kusisitiza kuwa kuna haja ya watu kubadili mtazamo walionao kuhusu suala la uchangiaji wa huduma za kijamii.
           

No comments:

Post a Comment