Friday, May 23, 2014

TFCG na AVA za kabili uharibifu wa mazingira Mvomero







 

SHIRIKA la kuhifadhi misitu ya asili Tanazani TFCG kupitia mradi wa  kuongeza thamani katika misitu AVA limeanza kuhamasisha jamii zinazoishi kando ya misitu kujiunga katika vikundi vya hisa kujipatia kipato na kuepuka uharibifu wa mazingira.

Hayo yameelezwa na Meneja wa Mradi wa AVA Bwana Hassan Chikira kwenye mapitio ya mradi unatekelezwa katika vijiji 31 wilayani Mvomero mkoa Morogoro.

Kwa mujibu wa Chikira vikundi hivyo kupitia mradi wa AVA vitawarahisishia kupata fedha za kuendesha miradi mingine na kuachana mpango wa kutumia maliasili misitu kama itega uchumi vyao katika maisha.

Mwenyekiti wa kikundi Benedict matei na Mwalimu wa kikundi cha hisa Shaban Mganga walisema kupitia vikundi hivyo wanakikundi sasa wanakoposheka na kuanzisha biashara na sghuguli ndogo ndogo za kuwaingizia kipato.
Mradi wa AVA umelenga kuhakikisha jamii inayozunguka misitu inaacha tabia ya kutumia misitu kama chanzo cha kipato chao na badala yake  kufanya shughuli nyingine na wanahifadhi misitu.


No comments:

Post a Comment