WAHUBIRI na wahadhiri wa
Dini ya kiiislam nchini wametakiwa kujikita katika kuhubiri Umoja na mshikamano
katika jamii na sio kuhubiri ubaguzi,uchochezi au kuletea mgawanyiko ambao
unaweza kujenga chuki miongoni mwa jamii na kusababisha taifa katika migogoro
na Vurugu.
Wito
huo Umetolewa na Naibu Mufti wa baraza kuu la waislam Tanzania(BAKWATA)Sheikh
Ali Muhiddini Mkoyogole wakati akifungua semina ya siku mbili ya wahadhiri na
wahubiri wa dini ya kiislam kutoka mikoa mbali mbali nchini iliyoandaliwa na
Taasisi ya kiislam ya Charity People Trust ambayo inajishughulisha na utoaji
huduma kwa jamii.
Amesema
Machafuko katika nchi mbali mbali yanatokana na maeno ya Uchochezi au mahubiri
yanayopandikiza chuki katika misingi ya dini,itikadi na baadae nchi hizo
hujikuta katika migogoro ya muda mrefu na hatimaye husababisha vita .
Kwa
upande wake Rais wa Taasisi hiyo Sheikh Abdallah Ndauka amesema madhumuni ya
kuandaa semina hiyo yanatokana na kuwepo kwa mgawanyiko na mahubiri
yanayokwenda kinyume na uislam ambayo yanaweza kupandikiza chuki katika jamii.
ujumbe muhimu sana hasa kwa wakati tulio nao,,, matatizo ya waislamu yana majawabu yake sio fujo,, pia kuna methodology yake ,,
ReplyDelete