Tuesday, June 17, 2014

AFISA tarafa aahidi kutokomeza unyanyasaji na unyanyapaa


Albino aliyenusurika kukatwa viungo mkazi wa Kilombero,Morogoro

AFISA tarafa ya Manispaa Morogoro Pakalapakala Mlenge,ameahidi kutokomeza unyanyasaji na unyanyapaa kwa wenye albino katika manispaa ya Morogoromji  licha ya bajeti inayotengwa dhidi ya mapambano hayo kuwa ndogo.

Akizungumza mwishoni mwa wiki wakati akifunga warsha ya  wenye ualbino Pakalapakala alisema ili timiza lengo Halmashauri na serikali zimeamua kufanya tathimini ya utambuzi changamoto zinazowakabili na kuzitafutia ufumbuzi.
Alisema serikali itaendelea kuwajali watu wenye albino kama walemavu wengine kwa kujitahidi kuzikabili changamoto zinazo wakabili hususani upatikanaji wa mafuta maalumu,kofia.miwani na mavazi yanayoendana na halia waliyonayo.

Aidha aliwataka kujishugulisha kutafuata wafadhili kwa kuandika andiko la mradi  kwenye mashirika mbalimbali wa ndani na nje ili kuziba pengo linalojitokeza pindi serikali inaposhindwa kutimiza lengo kutokanana uwezo wake kuwa mdogo.

Awali mwenyekiti wa chama cha watu wenye ualbino mkoani Morogoro David Mganga alimweleza afisa tarafa huyo kuwa bado halmashauri imeshindwa kutekeleza maazimio waliyokubaliana likiwemo la Afya na elimu kutolewa bure kwao.


No comments:

Post a Comment