Tuesday, June 17, 2014

WATU 20 wameuawa katika shambulizi Pwani ya Kenya


Askari wa Kenya wakipakia maiti ndani ya gari

WATU 20 wameuawa katika shambulizi la pili la usiku katika Pwani ya Kenya huku kundi la wapiganaji la Alshabaab limekiriki kutekeleza shambulizi hilo la pili katika vijiji viwili zaidi na kusema kuwa wengi ya waliouwa ni maafisa wa polisi.


Wapiganaji hao walivamia vijiji viwili karibu na mji wa Mpeketoni ,ambao ni eneo la mashambulizi ya kwanza ambayo yalisababisha mauaji ya watu 48.

Wakazi wa eneo hilo wamelalamikia serikali kwa kutowapa ulinzi baada ya shambulizi la kwanza na sasa wanaishi kwa hofu.

Serikali inasema kuwa wanamgambo wa Alshabaab walikata mawasiliano ya simu katika eneo hilo kabla ya kutekeleza shambulizi hilo.

Wanamgambo hao wanaohusishwa na kundi la Alqaeda wanasema kuwa wataendelea kufanya mashambulizi nchini Kenya ikiwa serikali haitaondoa wanajeshi wake nchini Somalia.

Shambulizi hilo la vijijini ni limeonekana kuwa mfumo mpya wa mashambulizi ambayo yamekuwa yakifanya na Al Shabaab ambalo mara nyingi limekuwa likilenga maeneo ya mijini hasa miji mikubwa.

Takriban watu 48 waliuawa katika mashambulizi yaliyofanyika usiku wa kuamkia Jumatatu huku washambuliaji wakishambulia hoteli na kituo cha polisi pamoja na kuteketeza magari.


No comments:

Post a Comment