Saturday, June 21, 2014

ASHIKILIWA na polisi kwa tuhuma za kuwaingilia kimwili watoto wenye umri chini ya miaka kumi


Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora Suzan Kaganda akiongea na waandishi wa habari

MKAZI wa kijiji cha Igurubi wilaya ya Igunga Mkoani Tabora  anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kuwaingilia kimwili watoto wenye umri wa chini ya miaka kumi baada ya kuwarubuni kwa kuwapa ubuyu na shilingi 500.


Hayo yamethibitishwa na kamanda wa polisi Mkoani Tabora SUZANA KAGANDA amesema tukio hilo limetokea hivi karibuni katika mtaa wa Muhaya kijiji cha Igurubi na kuntaja mtuhumiwa huyo kuwa ni SUDI SEIF mwenye umri wa miaka (47).

Kamanda  KAGANDA ameeleza kuwa mtuhumiwa huyo anadaiwa kuwatendea unyama watoto hao kwa kuwalaghai kuwapa ubuyu na pesa endapo wengekubaliana nae kufanya tendo la ndoa ambapo kwa kuwa watoto hao walikuwa wadogo alifanikiwa kuwashawishi  na alianza kwa kumchukua mtoto wa kwanza mwenye umri wa miaka (5) na miezi 4 anayesoma chekechea  shule ya msingi Igurubi.

Amesema akiwa chumbani na mtoto huyo alimwingilia kimwili katika sehemu zote za siri na kumsababishia maumivu makali hadi wazazi wake walipomgundua wakati aliporudi nyumbani muda wa jioni ambapo amedai baada ya tukio hilo kwa umri wa miaka 9 anayesoma darasa la pili shule ya msingi Ikonda kata ya Igurubi aliyemfanyia kama mtoto wa kwanza.
Aidha kamanda KAGANDA amesema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na kundi la wanakijiji nyumbani kwake na aliokolewa na askari polisi

No comments:

Post a Comment