![]() |
| Raisi Mteule wa Malawi Prof Peter Mutharika |
RAISI mteule wa
wa Malawi Prof Peter Mutharika anatarajiwa kufunga pingu
za maisha na mpenzi wake wa muda mrefu,mwishoni mwa wiki.,Imeelezwa
Taarifa hii ni kwa mujibu wa taarifa
kutoka ikulu ya Rais.
Kwa mujibu wa Taarifa toka Ikulu ya
nchi hiyo ni kuwa,: ''Ikulu ya Rais ina furaha kuwajulisheni kuhusu harusi ya
kitamaduni itakayofanywa kati ya Rais Arthur Peter Mutharika na mwandani wake
wa muda mrefu Madam Gertrude Hendrina Maseko.''
Taarifa hii iliwasilishwa na msemaji
wa Rais Chikondi Juma aliyesema kuwa sherehe ya harusi itakuwa ya faragha.
Rais Mutharika aliibuka mshindi
katika uchaguzi wa urais uliofanyika mwezi jana ambapo mshindani wake mkubwa
alikuwa rais aliyeondoka mamlakani Joyce Banda.
Rais Mutharika amewaambia maafisa wa
serikali kuhakikisha kuwa hakuna pesa za serikali zitatumiwa katika shughuli
hiyo.
Mutharika, mwenye umri wa miaka 74
na ambaye mkewe alifariki , ana watoto watatu, wasichana wawili na mvulana
mmoja.

No comments:
Post a Comment