![]() |
| Wakimbizi nchini Syria |
SHIRIKA la
kuwahudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR, linasema idadi ya watu
waliopoteza makao yao na kufanywa wakimbizi kutokana na vita ilizidi milioni
hamsini mwaka jana.
Idadi hii inasemekana kuwa kubwa
zaidi kuwahi kushuhudiwa tangu vita vya pili vya dunia.
Vita nchini Syria, ni moja ya sababu
kuu ya kuongezeka kwa idadi hiyo ya wakimbizi, lakini pia kuna mizozo mingine
katika Jamhuri ya Afrika ya Kati na nchini Sudan Kusini ambayo imechangia idadi
kubwa ya wakimbizi
Shirika la kuwahudumia wakimbizi la
UNHCR, linasema kuwa idadi hiyo ni ishara tosha ya athari za kukosa kuzuia
mizozo. Pia limesema kuwa mataifa tajiri yanapaswa kufanya juhudi kuhifadhi
wakimbizi hao.

No comments:
Post a Comment